Monday, 15 September 2014
DIWANI ALLY NKANGA WA CCM AJIUNGA NA CHADEMA
Diwani Ally Nkanga wa Singida Magharibi na Makamu
mwenyekiti wa Halimashauri ya wilaya ya Ikungi Singida Magharibi
amejiunga na chadema, na kukabidhiwa kadi ya Chadema kwenye mkutano wa baraza kuu la chadema linalofanya mkutano wake Mlimani City Dar Es Salaam. Chadema
inaendelea kubomoa ngome za CCM. Diwani huyo akizungumza mbele ya baraza
kuu, ameeleza kwamba CCM siyo sehemu salama tena, badala ya kuwatumikia
watanzania, wamewageuza watanzania kama kitega uchumi. Amesema chama
pekee ambacho kimeonyesha nia na dhamira njema, yenye kukidhi matarajio
na matamanio ya watanzania ni CHADEMA, na yeye kwa dhati kabisa, bila
kushawishiwa na mtu yeyote ameamua kuungana na timu ya ukombozi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment